Nafasi mpya za kazi NMB Bank
Nafasi mpya za kazi NMB Bank

Nafasi za Kazi 19 NMB Bank, Oktoba 2024

Nafasi za Kazi 19 NMB Bank; NMB Bank Plc, moja ya benki kubwa zaidi za kibiashara nchini Tanzania, inatafuta wataalamu wenye sifa kujaza nafasi mbalimbali. Benki ya NMB inatoa huduma za kibenki kwa wateja binafsi, wateja wa kibiashara wa kati na wadogo, huduma za serikali, mashirika makubwa, na mikopo kwa sekta ya kilimo.

Nafasi za Kazi 19 NMB Bank
Nafasi za Kazi 19 NMB Bank

Historia ya NMB Bank

NMB Bank ilianzishwa kwa mujibu wa Sheria ya Uanzishwaji wa Benki ya Taifa ya Microfinance ya mwaka 1997 baada ya kugawanywa kwa Benki ya Taifa ya Biashara (National Bank of Commerce – NBC). Hatua hiyo ya kisheria ilizaa mashirika matatu mapya:

  1. NBC Holdings Limited
  2. National Bank of Commerce (1997) Limited
  3. National Microfinance Bank Limited (NMB)

Kwa sasa, benki hii ina zaidi ya matawi 226, mawakala (wakala) zaidi ya 9,000, na mashine za ATM zaidi ya 700 kote nchini. NMB imejikita katika wilaya zote za Tanzania, ikiwa na wateja zaidi ya milioni 4 na wafanyakazi wapatao 3,400. NMB pia ni benki iliyoorodheshwa kwenye Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE). Wadau wakubwa wa hisa za NMB ni Arise B.V., yenye asilimia 34.9, na Serikali ya Tanzania yenye asilimia 31.8.

NMB Bank imepokea tuzo kadhaa zenye hadhi ya juu, ikiwa ni pamoja na:

  • Benki Bora Tanzania – Tuzo za Euromoney kwa miaka 8 mfululizo (2013-2020)
  • Benki Salama Tanzania – Tuzo ya Global Finance Magazine kwa mwaka 2020

Nafasi za Kazi NMB Bank – Oktoba 2024

NMB Bank inatoa nafasi hizi ili kuendeleza huduma zake kwa ubora wa hali ya juu na kuwafikia wateja katika sekta mbalimbali. Unaweza kusoma maelezo kamili ya nafasi hizi kupitia viungo vilivyo hapa chini.

Soma maelezo kamili kupitia link zifuatavyo:

Makala nyinginezo: